Assistant Researchers (7)

at Edrine Publishers
Location Dar es Salaam, Tanzania, United Republic of
Date Posted January 14, 2022
Category Management
Job Type Full-time
Currency TZS

Description

Description

Edrine PUBLISHERS ni watafiti,waandishi na wachapishaji wa vitabu mbalimbali vya ziada na kiada.

Tunafanya utafiti utakao pelekea kuandika na hatimaye kuchapisha kitabu kuhusu MTI WA MBAAZI PORI.

Tunatangaza nafasi za Kazi ya MTAFITI MSAIDIZI kwa waombaji wenye sifa zifuatazo:

  1. Elimu kuanzia kidato cha nne na kuendelea.
  2. Awe anaweza kusoma, kuongea na kuandika Kwa ufasaha lugha za Kiswahili pamoja na lugha ya Kiingereza.
  3. Awe anaishi katika mazingira au eneo ambako mti wa MBAAZI PORI unapatikana kwa wingi.
  4. Awe anaishi katika wilaya yoyote iliyopo Tanzania Bara au Tanzania visiwani ( Zanzibar).
  5. Awe na nafasi na muda wa kutosha kufanya Kazi ya utafiti usaidizi katika mradi huu Kwa Muda wa miezi Tisa mfululizo kuanzia mwezi FEBRUARI 2022 hadi mwezi NOVEMBA 2022
  6. Mwombaji akiwa na uzoefu ama ufahamu wa kutosha kuhusu MTI WA MBAAZI PORI atapewa kipaumbele.

IDADI YA NAFASI : NAFASI SABA ( 7)

MWISHO WA KUPOKEA MAOMBI NI TAREHE 30 JANUARI 2022.

Unapotuma Barua Pepe yako ya maombi, kwenye sehemu ya kichwa cha Barua Pepe ( SUBJECT) andika Jina la wilaya unayo ishi Kisha weka mabano halafu ndani ya mabano andika neno MBAAZI PORI.