Mhandisi Msanifu Majengo II (ARCHITECTS)
Location | Arusha, Tanzania, United Republic of |
Date Posted | December 18, 2020 |
Category | Engineering Government Management |
Job Type | Full-time |
Currency | TZS |
Description
JOB DETAILS:
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji anawatangazia Watanzania wote wenye sifa na nia ya kufanya kazi katika Jiji la Arusha kutuma maombi ya kazi ya muda kwa Mkurugenzi wa Jiji ndani ya siku 14 kuanzia tarehe ya Tangazo hili. Nafasi hizi ni za muda wa miezi sita kwa kazi zilizopangwa na kuidhinishwa na Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2020/2021. .
Sifa zinazotakiwa
Awe na Shahada/Stashahada ya juu ya Uhandisi kutoka vyuo vinavyotambuliwa na serikali katika fani za Uhandisi (Architects).
Job Skills: Not Specified
Kazi na Majukumu
• Kufanya kazi kwa vitendo katika fani ya usanifu majengo.
• Kufuatilia upatikanaji wa taarifa za taaluma za usanifu wa majengo.
• Kupitia mapendekezo ya miradi (Project proposals) mbalimbali ya majengo.
Applying Instructions
MAELEZO YA JUMLA
• Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na Mwenye akili timamu.
• Waombaji wawe na umri usiopungua miaka 18 na usiozidi miaka 45.
• Barua za maombi ziambatanishwe na nakala za vyeti vya Elimu/taaluma, cheti cha kuzaliwa na maelezo binafsi (CV).
• Mshahara utakuwa wa makubaliano kwa kuzingatia bajeti.
• Maombi yatakayotumwa kwa mkono hayatapokelewa.
• Waombaji wenye uzoefu wa kazi watapewa kipaumbele.
Maombi yatumwe kwa anuani ifuatayo:
Mkurugenzi,
Halmashauri ya Jiji la Arusha
S.L.P. 3013, Arusha.